Timu ya Serikali ya wanafuzi Chuo Cha Uhasibu Arusha-IAASO
chini ya Rais Wambura imepoteza mchezo wa mpira wa miguu wa ufunguzi wa michezo
ya wiki ya sherehe za kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza 2025/26 (IAA
FRESHERS’ WEEK).
Timu ya Baraza la Mawaziri iliyoungana pia na Wabunge (CRs) imepoteza
mchezo huo uliyochezwa leo 05 February, 2026 katika uwanja wa michezo IAA dhidi
ya timu ya watumishi wa chuo kwa
kufungwa magoli mawili kwa sifuri (2:0).
Kwa upande mwingine, timu ya wanafunzi wa Shahada wa mwaka
wa watatu (Bachelor III) imeibuka mshindi kwa kufunga magoli mawili kwa moja (2:1) katika
mechi yao dhidi ya timu ya wanafunzi wa ngazi ya Astashahada (Certificate).
