Timu za
mpira wa miguu za wanafunzi wa Chuo Cha Uhasibu Arusha-IAA kampasi ya Babati na
Arusha wameshiriki mchezo wa kirafiki wa mpira wa miguu katika viwanja vya
michezo kampasi ya Arusha, ikiwa moja ya burudani katika ziara yao waliofanya
katika kampasi ya Arusha.
Mchezo
huo umechezwa Januari 09, 2026 na timu zote ziliibuka na ushindi wa mabao
mawili (2:2), licha ya ushindani mkubwa wa kimchezo uliyoonesha uwanjani na
timu hizo.
Awali
alipozungumza na kituo cha televisheni cha IAA (IAA Media) rais wa IAA-kampasi
ya Babati Mhe. Tyson Mgaya aliahidi ushindi kwa timu yao, akisema wachezaji wao
wamejiandaa vya kutosha.
