Timu ya mpira wa miguu ya wanafunzi kutoka Chuo Kikuu Cha
Dodoma (UDOM) imekubali kupokea kichapo cha magoli 3 kwa 1 katika mchezo wao wa
kirafiki dhidi ya timu ya wanafunzi kutoka IAA-Arusha.
Akizungumzia kupoteza mechi hiyo, Kapteni wa timu ya UDOM
Ally Msabaha amesema mchezo una matokeo matatu kushinda, kufungwa na kupata
sale, wao wamekubaliana na kupoteza mchezo. Huku, baadhi ya wachezaji wake
wakilalamikia baadhi ya maamuzi ya refa wa mchezo.
Kwa upande wao timu ya IAA, iliyoibuka mshindi wa mechi kwa
kupata mabao 3, ikiongozwa na kocha Keba wamesema IAA ina vijana wenye vipaji na
mazoezi ya kila siku hivyo, kwa mechi ya muda wowote wapo tayari.
