HOTUBA
Rais wa serikali ya wanafunzi
Chuo Cha Uhasibu Arusha Mhe. Francis Wambura ametoa pole za dhati kwa Jumuiya
ya Wanyarwanda, manusura, na wote wanaoendelea kubeba maumivu na kumbukumbu za
Mauaji ya Kimbari dhidi ya Watutsi ya mwaka 1994 nchini Rwanda na kusema
kumbukumbu, mshikamano, na heshima inapaswa kutunza.
Mhe. Wambura amesema kufikiria
kuhusu tukio hilo, ni muhimu ili kuweza kujumuika na kuhakikisha vijana
wanakuwepo katika maeneo ya kumbukumbu. Hata hivyo, amesema ukichunguza kwa
undani historia ya Rwanda kabla ya 1994, wakati wa Mauaji ya Kimbari, na hata
baada yake, inakuwa wazi kwamba nafasi ya vijana si ya ishara tu ni ya msingi
kabisa.
However, when we look more
closely at the history of Rwanda before 1994, during the genocide against
Tutsi, and even in its aftermath, it becomes clear that the role of youth is
not symbolic, it is central.
Ikilinganishwa na hali ya sasa
ya eneo la Afrika Mashariki na dunia kwa ujumla, umuhimu wa vijana unaonekana
Zaidi, kwani ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pekee, takribani asilimia 65
ya watu wana umri wa chini ya miaka 35. Akiongeza kuwa vijana si kundi dogo la
kujumuishwa, wao ndio wengi wanaoamua mwelekeo wa jamii na hivyo si tu kwamba
ni sahihi bali ni lazima vijana wazungumze katika nyakati kama hizi si kama
nyongeza bali kama wajibu.
VIJANA KUYAFAHAMU HAYA.
Rais wambura ameendelea kusema
analizungumzia suala la mauaji si kama Mrwanda, bali kama kijana kutoka katika
ukanda wa Afrika Mashariki anayetambua fika kwamba anatoka nje ya historia hiyo
na hajapitia uzoefu uliounda yaliyopita ya Rwanda. Lakini kutokana na hilo,
vijana wanaweza kukutana na vipengele vya historia hiyo bila kuelewa uzito wake
kikamilifu, kwani kuna maneno ambayo hayabebi mara moja uzito wa kihisia.
Maneno yanayotafsiriwa moja
kwa moja yanaweza yasionyeshe hatari mara moja. Maneno ambayo awali hayakuwa na
maana hasi, bali yalizungumzia umoja. Lakini yalipoingizwa itikadi,
yalibadilishwa na hatimaye kuwa kitu tofauti kabisa, jambo ambalo linatoa funzo
muhimu kwa vijana wa leo.
This offer an important lesson
for us as youth that, what is dangerous is not always obvious at first.
Ideas,languages and identities can be gradually reshaped until they become
tools of division and harm. We must also confront the difficult truth that a
significant number of those who carried out acts of violence during genocide
were young people.
Kadhalika, Rais Wambura
amebainisha kuwa, mara nyingi vijana sio wapangaji wa mipango, bali husimama
katika nafasi ya utekelezaji wa yale yaliyopangwa na kuanzishwa tayari. Katika
historia ya vita, mauaji ya kimbari, na migogoro duniani kote, vijana mara
nyingi huwekwa mstari wa mbele katika vitendo vya vurugu.
Hata hivyo, ameendelea kuweka
wazi kuwa huenda si vijana wote nchini Rwanda walihusika, kwani mara nyingi
wapo vijana wanaopinga nia mbaya na vurugu hususani zinapotokea katika nchi. Hata
katika mauaji ya kimbari nchini Rwanda ya mwaka 1994, huenda walikuwepo vijana
waliokataa migawanyiko na waliochagua ujasiri badala ya hofu.
MCHANGO WA VIJANA
Rais Wambura amebainisha kuwa
inatambulika pia kwamba ukombozi na ujenzi upya wa Rwanda baada ya Mauaji ya
Kimbari ulifanywa kwa kiasi kikubwa na vijana, wengi wao waliokulia uhamishoni,
wakikabiliwa na changamoto, umaskini, na hasara, lakini wakiwa wameunganishwa
na maono ya mustakabali tofauti. Hali inayoonesha kwamba hata katika mazingira
yale yale ya maumivu, upungufu na simulizi hatarishi, bado chaguzi tofauti
zinawezekana na mara nyingi chaguzi hizo huathiriwa na mawazo na mazingira
yanayowazunguka watu.
Usahihi
wa historia
Rais Wambura amesema vijana
wengi waliopo hawakuwa hai mwaka 1994, kwani wengi historia hii si waliyoishi bali
wamejifunza. Historia ambayo inapitishwa kupitia familia, simulizi, elimu na
kwa kiwango kikubwa zaidi sasa kupitia majukwaa ya kidijitali.
Aidha amesema hali hii imeleta
fursa na hatari pia. Kwa upande mmoja, upatikanaji wa taarifa haujawahi kuwa
mkubwa, nafuu, na rahisi hivi. Vijana wanaweza kujifunza, kulinganisha
mitazamo, kushiriki mijadala, na hata kuhamasisha mabadiliko chanya na kwa
upande mwingine, majukwaa ya kidigitali yanaweza kupotosha ukweli kwa kuunda
mazingira ya sauti zinazofanana, kukuza ukweli nusu na kuinua sauti zisizo na
msingi wa ukweli.
Kwa wale ambao hawakushuhudia
historia moja kwa moja, kutofautisha kati ya ukweli na upotoshaji kunazidi kuwa
changamoto. Pia mienendo ya kutia wasiwasi duniani, ambapo itikadi hatarishi na
alama zake wakati mwingine zinachukuliwa kirahisi, kubadilishwa maana au
kuwasilishwa kwa namna inayozifanya zionekane za kawaida au hata kutokukubalika.
Rais Wambura ameweka bayana
kuwa kukanusha mauaji ya kimbari, kubadilisha historia na kusambaza simulizi za
uongo bado vinaendelea, kwa sababu zamani vilitegemea mifumo ya kati, sasa
vinaenea kwa kasi kupitia majukwaa yanayoendeshwa na algoriti, yanayopendelea
ushiriki hata kama yanakuza maudhui yenye mgawanyiko na hisia kali.
Je,
sisi kama vijana wa kimataifa tunaweza kufanya nini leo?
Rais Wambura amehitimisha kwa
kusema vinaja wanaweza kujitolea kulinda ukweli wa kihistoria, kukataa
kusambaza simulizi ambazo hazijathibitishwa, kupinga kukanusha na upotoshaji
popote vinapoonekana, kuhamasisha umoja katika jamii na kusimama pamoja si tu
kwa kumbukumbu bali kwa vitendo.
Hata hivyo, amesisitiza
kuchukua kumbukumbu hiyo katika namna watu wanavyofikiri, wanavyosema, na wanavyotenda
ili kauli ya “Haitatokea Tena” iwe uhalisia unaojengwa kwa vitendo, si ahadi inayorudiwa
tu.



