Serikali ya wanafunzi Chuo Cha
Uhasibu Arusha-IAASO imewapongeza waandaaji wa tamasha kubwa la ugawaji tuzo
kwa wanachuo wenye vipaji nchini Tanzania (Silent Ocean Uniawards)
linalofanyika IAA kwa mwaka huu.
Akizungumza kwa niaba ya rais
leo 24 April, 2026 katika semina ya "Kontena la Fursa", Mhe. Frank
Michael ambaye pia ni Waziri wa Habari na Mawasiliano amesema tamasha hilo ni
fursa na wanafunzi wa IAA wenye vipaji wamejiandaa vizuri kuhakikisha wanaibuka
washindi wa tuzo hizo.
Hata hivyo, leo wanafunzi wa
Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) wamepata fursa ya kushiriki semina maalum
iliyolenga kuwajengea uelewa kuhusu biashara na utambuzi wa fursa za kujipatia
kipato mtandaoni.
Kupitia semina hii ya leo
April 24, 2026, wanafunzi wamejifunza mbinu tofauti za kuanzisha na kuendesha
biashara, pamoja na uelewa wa njia bora za usafirishaji wa bidhaa, huku
wakisisitizwa umuhimu wa matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii kama nyenzo
muhimu katika kukuza biashara na kuongeza vipato vyao.
Semina hii iliyoandaliwa na
SILENT OCEAN UNIAWARDS kwa jina la “Kontena la Fursa,” imefanyika katika ukumbi
wa CH3 ndani ya Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) na imeshirikisha wanafunzi wa IAA
na wengine kutoka katika vyuo mbalimbali vilivyopo jijini Arusha.
Picha za matukio:





