RAIS WAMBURA APONGEZA DCEA NA IAA KUANDAA WARSHA

 

Rais wa Serikali ya Wanafunzi Chuo Cha Uhasibu Arusha-IAA Mhe. Francis Wambura ameipongeza Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya kanda ya kasikazini-DCEA pamoja na IAA, kwa kuandaa warsha ya kutoa elimu ya uhamasishaji wa kuzuia matumizi ya dawa za kulevya na uelewa wa afya ya akili.


Akizungumza Machi 6, 2026 katika ukumbi wa CH3-IAA wakati akitoa hotuba yake Rais Wambura amesema maadhimisho ya siku ya wanawake kimataifa ni ishara ya kuikumbusha jamii juu ya umuhimu wa wanawake katika maendeleo mbalimbali, akisema wanawake ni nguzo muhimu katika kujenga jamii yenya usawa, maendeleo na ustawi


Aidha, Rais Wambura ameongeza kuwa suala la matumizi ya dawa za kulevya pamoja na changamoto za afya ya akili ni masuala yanayohitaji umakini mkubwa, hasa kwa vijana na wamafunzi wote kushirikiana na kuhakikisha wanajenga mazingira salama yanayofanya watu kuwa na afya njema, nidhamu na malengo mema.


Kwa niaba ya serikali ya wanafunzi-IAASO Rais Wambura ameahidi kuendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali ikiwemo Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya-DCEA katika kuelimisha vijana na kuzuia matumizi ya dawa za kulevya pamoja na kujenga uelewa wa afya ya akili.