MAPOKEZI YA MGENI RASMI IAA FRESHERS' PARTY 2026

 

Kikao maalum cha mapokezi ya mgeni rasmi katika sherehe ya kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza kwa mwaka 2026, ndani ya Chuo Cha Uhasibu Arusha-IAA maarufu IAA WELCOME FRESHERS' PARTY.

Mapokezi haya yamefanyika katika ukumbi wa PGB tarehe 13 Februari, 2026 usiku, ambapo mgeni rasmi Mhe Halidi Mwinyi @mwinyi_halid ambaye ni Katibu Mkuu UVCCM Taifa alipokelewa rasmi.

Katika kikao hiki Mlezi wa Wanafunzi-IAA Nadhiru Abdulnuru amemkaribisha sana Halid Mwinyi katika sherehe hizo, na kusema yeye kama kijana ni mfano bora kwa vijana wa IAA ambao pia wana ndoto za kuwa viongozi wakubwa kitaifa.

Naye rais wa serikali ya wanafunzi-IAASO Francis Wambura amemshukuru Katibu Mkuu UVCCM Taifa mhe Halid Mwinyi kwa kukubali mualiko huo wa kuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo za usiku wa tarehe 13 Februari, 2026 katika viwanja vya michezo IAA.

Miongoni mwa viongozi waliohudhuria kikao na sherehe hizo ni Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Arusha, Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Arusha, Diwani wa Kata ya Engutoto, Marais na makamu wa rais wa vyuo mbalimbali mkoa wa Arusha (Tengeru, TUMA, ATC, IAA-Kampasi ya Babati nk), Mawaziri, manaibu mawaziri pamoja na makatibu wakuu wa wizara mbalimbali wa serikali za wanafunzi vyuoni na wageni wengine waalikwa.